Shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa OCHA limesema watu zaidi ya elfu 56 wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na operesheni kubwa za kijeshi zinazoendelea za kuukomboa mji wa Mosul kutoka kwa kundi la IS nchini Iraq. Robo tatu ya wakimbizi hao wanaishi kwenye kambi mbalimbali, huku wengine wakipokelewa na familia mbalimbali au kuishi kwenye majengo yasiyokamilika na makazi yasiyo rasmi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |