Idara ya forodha nchini Vietnam imekamata kilo 619 za pembe za Ndovu kutoka Afrika zilizokuwa zimefichwa katika makontena mawili mjini Chi Minh nchini humo.
Habari zinasema, wafanyabiashara za magendo wamebuni njia mpya za biashara hizo, ambapo safari hii pembe za Ndovu zilifichwa katika shehena za mbao, ili kuepusha ukaguzi wa mionzi.
Mkutano unaojadili biashara haramu za wanyamapori ulifanyika hivi karibuni huko Hanoi nchini Vietnam, ambapo wajumbe walijadili namna ya kuimarisha hatua za kupambana na magendo ya wanyamapori na bidhaa zinazotokana na wanyama hao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |