• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Polisi nchini Kenya watoa tahadhari kuhusu mipango ya mashambulizi ya Al-shabaab

    (GMT+08:00) 2016-11-30 09:45:42

    Polisi nchini Kenya wametoa tahadhari na kuimarisha usalama, kutokana na taarifa kuwa kundi la Al-shabaab linapanga kufanya mashambulizi nchini humo wakati wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

    Kamanda wa polisi wa Kenya Inspekta Jenerali Joseph Boinnet amesema kundi la Al-shabaab linapanga kukusanya wapiganaji wake katika eneo la Jedahaley nchini Somalia, na kuingia nchini Kenya kufanya mashambulizi kwenye maeneo ya mpakani na sehemu za utalii katika pwani ya Mombasa, wakiwalenga wana usalama na vyombo vya usafiri wa umma.

    Imefahimika kuwa baadhi ya wapiganaji wanapanga kujipenyeza kuingia Kenya kwa kujifanya wafugaji. Sehemu za mpakani zimetajwa kuwa na tishio kubwa la usalama.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako