• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yapeleka kikosi cha tatu cha askari wa miguu wa kulinda amani Sudan Kusini

    (GMT+08:00) 2016-12-05 18:12:22

    China imepeleka awamu ya kwanza ya askari 120 wa miguu kati ya 700 wa kikosi cha kulinda amani katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba.

    Walinda amani hao walipata mafunzo maalum ya miezi mitatu ya kulinda amani na watakuwa na majukumu ya kulinda raia, kusaidiana na Umoja wa Mataifa katika majukumu ya kulinda haki za binadamu na kufanya doria.

    Kikosi hiki ni cha 3 kwenda Sudan Kusini tangu kikosi cha kwanza cha kulinda amani kupelekwa mwaka 2015. Mwezi Julai mwaka huu, askari wawili wa kulinda amani wa China waliuawa na watano kujeruhiwa wakati wa kulinda amani mjini Juba.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako