Kampuni ya serikali ya kuzalisha umeme Kengen imetangaza mradi mkubwa wa mabilioni ya fedha wa kurekebisha kituo cha kuzalisha umeme cha Eburru ili kuongeza uzalishaji wake ndani ya kipindi cha miaka miwili.
Kengen imesema mipango hivi sasa inaendelea kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka megawati 2.4 hadi megawati 25 kati ya mwaka wa 2018 na 2019. Kengen imeongeza kuwa inapanga kuchimba visima vingine ili kufikia lengo hilo ndani ya miaka miwili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |