Mwenyekiti wa chama cha PLO ambaye pia ni rais wa Palestina Bw. Mahmoud Abbas amesema tume hiyo itachukua hatua halisi ili kumaliza ukaliaji wa ardhi yake unaofanywa na Israel.
PLO kimesema tume hiyo itafuata azimio namba 2334 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, linalotoa mwito kwa Israel kuacha kujenga na kupanua makazi yake katika ardhi iliyotwaa mwaka 1967.
Wiki iliyopita wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa walipiga kura na kupitisha azimio la kuilaani Israel kukalia ardhi ya Palestina, na kutoa wito kwa Israel isimamishe vitendo hivyo. Nchi 14 zilipiga kura ya ndio.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |