Shirika la Mpango wa chakula duniani WFP limesema zaidi ya watu milioni 3 wanahitaji msaada wa kibinadamu kwenye sehemu za mashariki mwa Ukraine, na shirika hilo litaendelea kuwasaidia watu laki 2.2 kwenye maeneo yenye migogoro nchini humo kwa mwaka huu. WFP imekuwa inatoa msaada wa dharura wa chakula Mashariki mwa Ukraine kuanzia mwaka 2014 na kuwafika watu laki 8.5. Shirika hilo limesema litaendelea kusambaza chakula kwa watu elfu 70 kwenye maeneo hayo mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |