• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yawekeza zaidi ya dola za kimarekani bilioni 50 katika nchi za "Ukanda Mmoja, Njia Moja"

    (GMT+08:00) 2017-03-06 19:05:57

    Mkurugenzi wa Kamati ya maendeleo na mageuzi ya taifa la China Bw. He Lifeng leo hapa Beijing amesema, katika miaka mitatu iliyopita, uwekezaji uliofanywa na China katika nchi za Ukanda wa kiuchumi wa Njia ya Hariri na Njia ya Hariri Baharini umezidi dola za kimarekani bilioni 50.

    Bw. He amesema ujenzi wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" unaendelea kwa kasi, pia umepata mafanikio makubwa kuliko ilivyotarajiwa. Amesema pendekezo la China kuhusu "Ukanda Mmoja, Njia Moja" limeungwa mkono na zaidi ya nchi na mashirika ya kimataifa 100, na China imesaini makubaliano mbalimbali ya ushirikiano na serikali za nchi nyingine, na makubaliano kadhaa ya ushirikiano na mashirika ya kimataifa.

    Bw. He pia amejulisha kuwa mkutano wa kilele wa ushirikiano wa kimataifa kuhusu "Ukanda mmoja na Njia moja" utafanyika hapa Beijing mwezi Mei mwaka huu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako