• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bunge la umma la China lajadili ripoti ya kazi kuhusu Kamati ya kudumu ya bunge la umma la China

    (GMT+08:00) 2017-03-08 19:31:15
    Mkutano wa 5 wa bunge la umma la China la awamu ya 12 unaendelea hapa Beijing, ambapo bunge hilo limekagua na kujadili ripoti ya kazi ya Kamati ya kudumu ya bunge la umma la China iliyowasilishwa leo.

    Katika ripoti hiyo, spika wa bunge la umma la China Bw. Zhang Dejiang amesema, mwaka jana Kamati ya kudumu ya bunge la umma la China ilitilia mkazo katika miradi muhimu inayohusu mageuzi, maendeleo na utulivu, kuboresha ubora wa utungaji wa sheria, na kutekeleza hatua kwa hatua sheria kadhaa muhimu. Amesema mwaka huu, kamati hiyo itarekebisha sheria ya usimamizi wa kiutawala kuwa kuwa sheria ya usimamizi ya taifa, na pia sheria mbalimbali zinazohusu jamii, utamaduni na ikolojia zitatungwa au kukamilishwa. Bw. Zhang Dejiang pia amesisitiza kuwa kazi kuu ya kamati hiyo mwaka huu itakuwa ni kukamilisha mfumo wa sheria kwa kufuatia mfumo mpya wa maendeleo wa China.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako