• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Sera ya China moja ni msingi wa uhusiano baina ya China na Marekani

    (GMT+08:00) 2017-03-15 11:39:46
    Waziri Mkuu wa China Li Keqiang amesema kuwa sera ya China moja itaendelea kuwa msingi wa uhusiano kati ya China na Marekani.

    Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa mwaka wa Bunge la Umma la China, Li amesema Rais wa China Xi Jinping na mwenzake Rais wa Marekani Donald Trump walifanya mazungumzo kwa njia ya simu mara baada ya Trump kuingia madarakani, ambapo viongozi hao wawili wamekubaliana kuendeleza uhusiano baina ya nchi hizo mbili.

    Li amebainisha kuwa Rais wa Marekani na Viongozi waandamizi kutoka katika utawala wake wamekubaliana kuwa Marekani itaendelea kufuata sera ya China moja.

    Ameongeza kuwa sera hii imefanya msingi mzuri usiotetereka wa ushirikiano kati ya China na Marekani licha ya kubadilika kwa mazingira, na kusema kuwa msingi huu hautodhoofishwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako