Matokeo hayo yanamaanisha Yanga inatolewa kwa bao la ugenini, baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. ZANACO FC wao wametinga hatua ya makundi na Yanga itawalazimu kusubiri droo ya kombe la Shirikisho ili kujua watakutana na timu gani.
Timu nyingine ya Tanzania, Azam FC imetupwa nje ya michuano ya kombe la Shirikisho baada ya kufungwa na wenyeji Mbabane Swallows goli 3-0 nchini Swaziland.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |