Viongozi wa Afrika wamepitisha azimio la kuongeza juhudi za kukusanya raslimali zaidi ili kuliwezesha bara hilo kujitegemea.
Kwenye taarifa baada ya mkutano wa kwanza wa Kiuchumi wa Afrika uliofanyika nchini Mauritius, viongozi hao walisema itakuwa vigumu kufikia lengo la Umoja wa Afrika la mwaka wa 2063 iwapo hakutakuwa na mapato ya kutosha na kujitegemea kwa nchi za Afrika.
Walitoa wito pia wa kuwa na sheria ya pamoja ya kupiga marufuku uuzaji wa mali ghafi za Afrika bila kuongea dhamani na wakati huo huo kuondoa vikwazo vya usafirishaji wa watu na bidhaa barani humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |