Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje wa China Bibi Hua Chunying amesema, mjumbe maalumu wa serikali ya China kuhusu suala la Syria Bw. Xie Xiaoyan atahudhuria duru ya 5 ya mazungumzo ya amani kuhusu suala la Syria itakalofanyika huko Geneva.
Hua amesema, Bw. Xie ataendelea kuhimiza mazungumzo ya amani, na kufanya juhudi na mchango wa kimkakati kwa utatuzi wa suala la Syria.
Duru ya 5 ya mazungumzo ya amani kuhusu suala la Syria inatarajiwa kufanyika kesho huko Geneva, Uswisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |