Benki ya dunia imetangaza kwamba itatoa mikopo ya dola bilioni 57 kwa nchi zilizoko chini ya Jangwa la Sahara ndani ya miaka mitatu ijayo.
Benki hiyo imesema dola bilioni 45 zitatoka kwenye shirika la maendeleo la kimataifa IDA ambalo ni la benki hiyo linalotoa mikopo bila riba kwa nchi maskini duniani.
Mkopo huo pia itajumuisha pesa zingine dola biloni nane za uwekezaji wa sekta ya kibinafsi ambazo zitatoka kwa shirika la fedha la kimataifa IFC.
Maafisa wanasema mkopo huo utatumika kuendeleza miradi ya maendeleo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |