• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • LA LIGA: Barca yapigwa, Neymar apewa kadi nyekundu

    (GMT+08:00) 2017-04-10 08:23:38

    Barcelona wameshindwa kukaa kileleni mwa La Liga baada ya kukubali kichapo cha bao 2-0 na Malaga katika uwanja wa La Rosaleda.

    Bao za Malaga zilifungwa na Sandro na Jony kwenye Dakika za 32 na 90. Barca walibaki mtu 10 kuanzia dakika ya 65 baada Neymar kupewa kadi nyekundu kwa rafu mbaya.

    Matokeo hayo yamewaacha Barca katika nafasi ya pili wakiwa pointi 3 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Real Madrid ambao wana mechi moja mkononi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako