MKUU wa Mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi ameziagiza mamlaka zinazohusika na kusimamia rasilimali zinazopatikana mkoani humo hasa madini kuhusisha wananchi wa huko ili wanufaike.
Aidha anasema kumekuwepo na wachimbaji wa madini ya dhahabu, shaba na vito vingine vingi lakini wananchi waliopo kwenye maeneo ya migodi hiyo hawajaweza kunufaika na uchimbaji huo.
Hivyo kuanzia sasa mamlaka zinazohusika hazina budi kulinda na kusimamia kikamilifu uchimbaji wa madini hayo ili uweze kunufaisha wakazi wa hapa.
Kwani Uchimbaji madini mkoani hapa haujaleta manufaa yoyote.
Katika kikao hicho, wajumbe wengi walishauri pawepo na masharti ya kila mgodi kuwa na mashine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |