• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kibarua cha kocha wa Asante Kotoko ya Ghana chaota mbawa

    (GMT+08:00) 2017-04-12 09:52:30
    Kocha wa zamani wa vilabu vya Simba ya Tanzania, Gor Mahia na AFC Leopard za Kenya Zdravko Logarusic amevunja mkataba na klabu ya ligi kuu ya Ghana, Asante Kotoko. Kotoko wamethibitisha kuwa wamevunja mkataba na Mcroatia huyo, kwa makubaliano, baada ya kumpa kibarua, kilichodumu kwa miezi mitatu tu.

    Siku za hivi karibuni, Loga alizuiliwa na mashabiki wa timu hiyo kuendesha mazoezi kwa madai ya kutoridhishwa na mbinu za kocha huyo, kufuatia timu kutoka sare na Inter Allies.

    Loga aliiongoza klabu hiyo ya Ghana michezo 11, ambapo alishinda michezo mitano, akatoka sare minne na kupoteza miwili.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako