Benki kuu ya Uganda imesitisha oparesheni za vituo vya kubadilisha pesa zinazomilikiwa na mfanyabiashara Sudhir Ruparelia.
Vituo hivyo ambavyo ni pamoja na Crane Forex Bureau ambavyo ni mojawepo wa vile vya zamani mjini Kampala vilikatazwa kupewa leseni upya kwa tuhuma za kukosa kuwajibika kulingana na sheria.
Leseni yake ilikuwa imeisha muda wa matumizi Desemba 2016.
Gavana wa benki kuu ya Uganda Emmanuel Tumusiime-Mutebile ameonya wananchi dhidi ya kubadilisha pesa kwenye vituo hivyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |