• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kombe la Shirikisho barani Afrika: Safari ya Yanga ya Tanzania yafika tamati

    (GMT+08:00) 2017-04-17 08:47:38
    Safari ya Yanga katika michuano ya Afrika leo imefikia tamati baada ya kufungwa mabao 4-0 na Mouloudia Club Alger Uwanja wa Julai 5, 1962 mjini Al-Jaza'ir, Algiers, Algeria katika mchezo wa marudiano wa mchujo wa kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

    Kwa matokeo hayo, Yanga inatolewa kwa jumla ya mabao 4-1 baada ya kushinda 1-0 katika mchezo wa kwanza Dar es Salaam wiki iliyopita, bao pekee la kiungo Mzimbabwe, Thabani Kamusoko.

    Katika mchezo huo uliochezeshwa na marefa wa Guinea, Yakhouba Keita aliyesaidiwa na Aboubacar Doumbouya na Mamady Tere, hadi mapumziko, wenyeji walikuwa mbele kwa mabao 2-0.

    Wakati refa Yakhouba Keita anajiandaa kupuliza kipyenga cha kuhitimisha mchezo huo, Awady Said akaifungia MC Alger bao la nne akitumia makosa ya mabeki wa Yanga, Kevin Yondan na Hassan Kessy kuchanganyana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako