Pamoja na kufungiwa mchezaji huyo, timu yake imenyang'anywa ushindi na kupewa timu ya jogoo kutokana na kosa hilo. Jogoo ilipeleka malalamiko kwenye chama cha mpira wa kikapu mkoa wa Dar es salaam (BD) ambao ni wasimamizi wa ligi ya RBA, kuwa Joseph ni mchezaji wao na wanashangaa kuichezea DB Young Stars.
Mkurugenzi wa ufundi wa chama cha mpira wa kikapu Haleluta Kavambi amethibitisha kufungiwa kwa mchezaji huyo na kusema adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa wachezaji wote wanaoshiriki ligi ya RBA.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |