Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM leo kimesema kimechunguza kifo cha askari wake katika mji wa Bula-burte, jimbo la Hiiraan, katikati mwa Somalia.
Askari huyu mwenye uraia wa Djibouti aliuawa na mwenzake kutoka jeshi la Somalia baada ya mabishano.
Msemaji wa AMISOM Wilson Rono amethibitisha tukio hilo, na kusema kuwa uchunguzi umefanywa ili kujua sababu ya mabishano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |