Shirika la kukadiria ubora wa bidhaa nchini Kenya (KEBS) limelalamikia kuongezeka kwa bidhaa ambazo hazifikia ubora unaohitajika.
Mkurungezi wa shirika hilo Charles Ongwae ametoa wito kwa wafanyabiashara kuzingatia viwango vilivyowekwa na serikali kabla ya kuagizia bidhaa kutoka nje.
Alisema bidhaa zinazoingia Kenya lazima zikaguliwe kutoka nchi zinakonunuliwa na pia zinapoingia nchini.
Amesema wameagiza maduka yote kutonunua bidha ambazo hazina vibandiko vya ukaguzi na ubora na pia kuwataka wakenya kuwa waangalifu.
KEBS imesema Kenya ndio inayoongoza kwa kuwa na bidhaa nyingi gushi katika kanda ya Afrika Mashariki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |