Kamati ya utalii ya Zimbabwe imesema, safari za ndege za moja kwa moja kutoka Nairobi hadi maporomoko ya maji ya Victoria zilizozinduliwa na shirika la ndege la Kenya zitastawisha utalii katika eneo hilo.
Mkuu wa baraza la utalii la Zimbabwe Bw. Tich Hwingwiri amesema, shirika la ndege la Kenya litaanza safari hizo mwezi ujao, akiongeza kuwa sekta ya utalii itanufaika kutokana na safari hizo.
Bw Hwingwiri pia amesema, mashirika mengi zaidi ya kimataifa yatazindua safari ya kuelekea maporomoko ya maji ya Victoria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |