• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Raia 715 wauawa katika mapigano Afghnistan robo ya kwanza ya mwaka huu

    (GMT+08:00) 2017-04-28 12:58:43
    Taarifa iliyotolewa na Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA imesema katika robo ya kwanza ya mwaka huu, mapigano nchini humo yamesababisha vifo vya raia 715 na wengine 1,466 kujeruhiwa.

    Taarifa pia inaonyesha kuwa asilimia 62 ya matukio yaliyosababisha vifo na majeruhi yalipangwa na wapiganaji wanaopinga serikali, kiasi ambacho kimeongezeka kwa asilimia 5 ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huo. mabomu na milipuko ya kujitoa muhanga bado ni njia kuu zinazosababisha vifo na majeruhi zaidi kwa raia.

    Eneo lenye wahanga wengi zaidi ni mkoa Kabul, ukifuatiwa na mkoa wa Helmand, Kandahar na Nanagarhar. Mashambulizi mengi yaliwalenga watumishi wa serikali, wazee wa makabila na wafanyakazi wa mashirika ya kibinadamu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako