Askari wapatao 80 wa Uingereza wamefika nchini Sudan Kusini kutoa uungaji mkono wa kiufundi na kimatibabu kwa tume ya Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS. Tume hiyo imesema kati yao wanajeshi wa huduma za matibabu watatekeleza majukumu yao kwenye vituo vya kuhifadhi raia vya Malakal na Bentiu, na hospitali ya ngazi ya pili huko Bentiu, huku wahandisi wakishughulikia kazi ya kuboresha miundombinu kwenye kambi za tume hiyo ya Umoja wa Mataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |