Wakulima wa miraa katoka eneo la Igembe Kusini hapa nchini Kenya wameingiwa na hofu baada ya mazao yao kukaushwa na viwavi waharibifu.
Mwakilishi wa Shirika la Utafiti wa Kilimo na mifugo nchini Kenya Bi Rahab Magoti, amesema kwamba inawezekana viwavi hao wameshambulia miraa kwa sababu mimea mingine katika eneo hili imeharibiwa na watu.
Bi Magoti amewaambia wakulima katika eneo la Aithiru Gaiti kuwa ni vigumu kwa Shirika la Utafiti wa Kilimo kuufanyia utafiti mmea wa miraa kwa sababu mmea huo haukuwa umeorodheshwa kama zao la kibiashara la kitaifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |