Rais Trump alisema hayo wakati alipozungumza kupitia televisheni pamoja na rais Mahmoud Abbas wa Palestina ambaye yuko ziarani nchini Marekani.
Rais Trump pia amesema, nchi yoyote ikiwemo Marekani haiwezi kuzilazimisha Israel na Palestina zifikie makubaliano, na kwamba nchi hizo mbili zinapaswa kufanya juhudi kutimiza lengo hilo litakalozisaidia pande hizo mbili kuishi na kustawi kwa pamoja.
Kwa upande wake, Rais Abbas alisema kuwa, anaamini kuwa Palestina na Israel zinawezekana kufikia makubaliano ya kutatua mgogoro kati yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |