Russia, Iran na Uturuki zimesaini makubaliano ya kuanzisha maeneo salama nchini Syria.
Makubaliano hayo yanalenga kusimamisha mapambano, kuboresha hali ya kibinadamu, na kutoa mazingira yanayohimiza mchakato wa amani na ufumbuzi wa kisiasa wa mgogoro wa Syria.
Habari zinasema, ingawa serikali ya Syria inaunga mkono mpango huo, makundi ya upinzani ya Syria yameukataa, na kusema makubaliano hayo yatatishia ukamilifu wa ardhi ya Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |