Takwimu zilizotolewa na tume ya uchaguzi ya Korea Kusini zinaonyesha kwamba Bw Moon Jae-in kutoka Chama cha Kidemokrasia amechaguliwa kuwa rais mpya wa Korea Kusini.
Kati ya asilimia 88.7 ya kura zilizohesabiwa Bw Moon Jae-in amepata asilimia 40.3 na kufanyikiwa kumshinda mpinzani wake Bw Hong Joon-pyo na kuthibitishwa kuwa rais mpya wa Korea Kusini. Wagombea wengine Bw Ahn Cheol-soo na Bw Hong Joon-pyo wamekubali kushindwa.
Habari zinasema Bw Moon Jae-in ataanza kazi mara moja baada ya kupata uthibitisho kutoka kwa tume ya uchaguzi.
Ikulu ya Marekani imempongeza Bw Moon Jae-in kwa ushindi wake na kusema itashirikiana na Korea Kusini chini ya uongozi wa Bw Moon Jae-in.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |