Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei amesema nchi yake itaendelea kuimarisha uwezo wa makombora. Ayatollah amesema hayo alipokutana na kamanda wa Kikosi cha ulinzi wa mapinduzi ya kiislamu. Amesema makombora iliyo nayo Iran yanaweza kushambulia kwa usahihi shabaha zilizo umbali wa maelfu ya kilomita, na kusisitiza kuwa nguvu ya kijeshi ya Iran ni chombo cha kujilinda kilichoendelezwa kwa kujitegemea, na pia ni mbinu muhimu ya kulinda usalama wa taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |