Rais Uhuru Kenyatta amezihimiza serikali za nchi za Afrika kuimarisha mashirika ya bima ili kusaidia kuunga mkono biashara ndani ya bara hilo.
Kwenye hotuba yake iliyosomwa na waziri wa fedha Bw. Henry Rotich kwenye mkutano mkuu wa 17 wa Bima ya Biashara ya Afrika ATI, rais Kenyatta pia amezitaka serikali za nchi za Afrika kufikiria uanachama wa ATI.
Rais Kenyatta amesema, nchi za Afrika zimesaini Makubaliano ya Biashara Huria ya Bara hilo, kwa lengo la kuhimiza ukuaji wa biashara kati ya nchi za Afrika, pamoja na kuzisaidia nchi za bara hilo kunufaika na biashara ikiwa nguvu ya ukuaji na maendeleo endelevu.
ATI inafanya kazi ya kuhimiza biashara za ndani na nje ya bara hilo kupitia mfumo wake wa kupunguza hatari, na kuwapatia uhakikisho wawekezaji wa ndani na nje.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |