Zaidi ya waasi elfu moja wa Syria wameondoka maeneo ya kaskazini mashariki ya mwa mji mkuu Damascus, na kuelekea maeneo yaliyoko kaskazini mwa nchi hiyo yanayodhibitiwa na waasi. Jeshi la Syria limesema baada ya operesheni za kijeshi zilizodumu kwa miezi minne, jeshi la serikali limekomboa maeneo ya kaskazini mashariki mwa Damascus, na waasi kwenye maeneo hayo wamejisalimisha na watahamishiwa kwenye maeneo ya kaskazini mwa Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |