Wataalamu wa nchi za Afrika wamekutana nchini Uganda kujadili na kutunga sera ya pamoja ya Afrika kuhusu uhamiaji. Hotuba ya rais Yoweri Museveni wa Uganda iliyosomwa kwenye ufunguzi wa mkutano huo inasema, uhamiaji ni suala linalofuatiliwa kote duniani, na linatakiwa kushughukiwa kwa njia ya kibinadamu. Amesema Afrika ina raslimali nyingi kwa hivyo watu wa bara hilo hawapaswi kufa wakijaribu kuvuka bahari ya Mediterranean, kwa matumaini ya kutafuta maisha bora barani Ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |