Kampuni ya Ernst&Young imetoa ripoti ya mwaka 2017 kuhusu uwezo wa Afrika wa kuvutia uwekezaji ikionesha kuwa, mwaka jana Afrika ilivutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni katika miradi 676, ambayo ni pungufu kwa asilimia 12.3.
Ripoti hiyo imesema, fedha zilizotokana na uwekezaji huo ziliongezeka kwa asilimia 31.9 kutokana na uhimizaji wa sekta za majengo, hoteli, mawasiliano na usafirishaji.
Afrika Kusini ilivutia miradi mingi ya uwekezaji, na Morocco, Misri, Nigeria na Kenya zilichukua asilimia 58 ya idadi ya miradi ya uwekezaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |