• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya zajadilia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na usalama

    (GMT+08:00) 2017-05-19 09:36:02
    Mkutano wa mawaziri wa ulinzi wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya uliofanyika jana huko Brussles umefikia makubaliano juu ya kuimarisha ushirkiano wa ulinzi na usalama.

    Akikutana na waandishi wa habari baada ya mkutano huo, mjumbe mwandamizi wa sera za usalama na mambo ya nje Bi. Federica Mogherini alisema chini ya mfumo wa sera ya pamoja ya ulinzi na usalama, nchi wanachama wa umoja huo zimepata maendeleo katika kuboresha muundo wa usimamizi wa migogoro, kuhimiza ushirikiano wa kiusalama na nchi washirika na mashirika ya kimataifa, kuinua uwezo wa jeshi wa kukabiliana na hali ya dharura na kuimarisha udhibiti wa migogoro ya kiraia. Amesema nchi hizo zimekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano katika eneo hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako