Akikutana na waandishi wa habari baada ya mkutano huo, mjumbe mwandamizi wa sera za usalama na mambo ya nje Bi. Federica Mogherini alisema chini ya mfumo wa sera ya pamoja ya ulinzi na usalama, nchi wanachama wa umoja huo zimepata maendeleo katika kuboresha muundo wa usimamizi wa migogoro, kuhimiza ushirikiano wa kiusalama na nchi washirika na mashirika ya kimataifa, kuinua uwezo wa jeshi wa kukabiliana na hali ya dharura na kuimarisha udhibiti wa migogoro ya kiraia. Amesema nchi hizo zimekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano katika eneo hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |