Korea Kaskazini imethibitisha kuwa imefanya jaribio la kurusha kombora lingine la masafa ya kati aina ya "Pukguksong-2" Jumapili, ikiwa ni mara ya pili kwa nchi hiyo kufanya majaribio ya makombora ndani ya wiki moja. Shirika la habari la Korea kaskazini limesema rais Kim Jong Un wa nchi hiyo alishuhudia jaribio hilo na kwamba linalenga kupima vigezo na uwezo wa kombora hilo katika hali tofauti ya kivita, kabla ya kutumiwa rasmi na jeshi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |