Rais Recep Erdogan wa Uturuki amechaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa chama tawala cha nchi hiyo AKP, baada ya marekebisho ya katiba yaliyopitishwa Aprili kwenye kura za maoni kumruhusu aendelee kuwa na wadhifa huo. Shirika la habari la Uturuki limesema chama hicho kiliitisha mkutano maalumu Jumamosi mjini Ankara kwa ajili ya kumchagua mwenyekiti mpya, ambapo rais Erdogan akiwa mgombea wa pekee alichaguliwa kwa kupata asilimia 96 ya kura.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |