Uchunguzi mpya wa maoni unaonesha kuwa kiwango cha wananchi wa Ufaransa kuridhika na rais mpya Emmanuel Macron na waziri mkuu mpya Édouard Philippe ni asilimia 62, na asilimia 55 mtawalia. Kabla ya hapo uchunguzi uliofanywa na kampuni ya Elabe ulionesha kuwa asilimia 45 tu ya wahojiwa wana imani na rais Macron, kiwango ambacho ni chini kuliko marais waliopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |