Timu ya raga ya Shujaa ya Kenya imetupwa nje ya michuano hiyo baada ya kukubali kichapo cha 47-0 toka kwa Marekani katika mechi za kundi A za michuano hiyo inayofanyika mjini London.
Katika mechi ya ufunguzi jijini London, Kenya ilitupa uongozi na kuzidiwa na miamba Afrika Kusini kwa pointi 12-10. Baada ya vichapo hivyo viwili, mashabiki wamejitosa katika mitandao ya jamii kuzishambulia kwa maneno makali timu ya Shujaa pamoja na Shirikisho la mchezo wa Raga la Kenya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |