Timu taifa ya kriketi ya Uganda leo haipaswi kufanya makosa itakapotupa karata yake dhidi ya timu ya taifa ya Singapore katika michuano ya ligi ya dunia ya kriketi (WCL) mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Entebbe.
Kocha wa timu wa timu hiyo Steve Tikolo anakiri kuwa mchezo huo utakuwa mgumu kutokana na kuwa timu pinzani wanayokutana nayo ni nzuri na ina uzoefu wa kutosha lakini watapambana ili kupata ushindi.
Kesho timu hiyo itavaana na timu ya taifa ya Malaysia, ambapo katika mchezo uliochezwa jana, Malaysia iliifunga Singapore.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |