Miaka michache mingi Rwanda imejaribu kuongeza mauzo ya nje, hasa katika maua, mboga, na matunda, lakini jaribu hilo limekubwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ada ya juu ya kusafirisha mizigo inayotozwa na mashirika ya ndege na masuala mengine kama vile ukosefu wa vifaa vya baridi.
Kulingana na wawekezaji katika sekta hiyo ni kwamba vikwazo vya juu vimezuia mipango ya nchi ya kukuza mauzo ya nje na thamani ya kilimo cha maua kwa sababu inafanya bidhaa kuwa na ushindani wa chini kwenye soko la kimataifa.
Lakini kulingana na bodi ya taifa ya mauzo ya nje ya bidhaa za kilimo (NAEB) ni kwamba suala hili la ada za juu inaweza kuwa historia baada ya baadhi ya mashirika ya ndege kusema watapunguza ada zao kwa karibu nusu ya ada ya zamani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |