Katibu wa wizara ya mambo ya ndani wa Libya Abdossalam Ashour amelaani shambulizi la bomu lililotokea Manchester na vitendo vyote vya kigaidi vinavyowalenga raia.
Ashour amesisitiza umuhimu wa kushirikiana na Uingereza kutafuta mitandao ya kigaidi iliyohusika katika shambulizi hilo. Amesema waziri mkuu wa Libya Fayez al-Sarraj amemuhakikishia mwenzake wa Uingereza Bi. Theresa May, na kusisitiza kuongeza mawasiliano na uratibu kati ya nchi hizo mbili katika kupambana na ugaidi.
Amesema Libya haiwezi kukaa kimya katika mapambano dhidi ya ugaidi, na itasimama thabiti kuunga mkono juhudi za kutokomeza ugaidi, katika ngazi ya taifa au ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |