Fainali hii ilichezwa huko Vicente Calderon Jijini Madrid na ndio mechi ya mwisho kabisa kwa kocha wa Barca Luis Enrique ambae anaondoka klabuni hapo.
Barca walitangulia kufunga dakika ya 30 kupitia Lionel Messi na Alaves kusawazisha kwa Frikiki ya Theo Hernandez Dakika ya 33. Barca walipiga bao 2 za chapchap dakika za 45 na 48 kupitia Neymar na Alcarer na kwenda Haftaimu 3-1 mbele.
Hii ni mara ya 3 mfululizo kwa Barca kutwaa Kombe hili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |