Muingereza Mohamed Farah alitwaa ubingwa kwa dakika 13:00.70 nao Yomif Kejelcha kutoka Ethiopia (13:01.21) na bingwa mara mbili wa nusu-marathon duniani Kamworor (13:01.25) waliridhika katika nafasi za pili na tatu.
Ronald Kwemoi naye alitimka kasi ya juu mwaka huu wa 2017 aliposhinda mbio za maili moja kwa dakika 3:49.04. Aliongoza Wakenya Elijah Manangoi (3:49.08), Timothy Cheruiyot (3:49.64) na Vincent Kibet (3:51.17) kumaliza katika nafasi nne za kwanza.
Bethwell Birgen aliridhika katika nafasi ya tisa (3:53.50), Silas Kiplagat wa 12 (3:57.59) naye bingwa wa Olimpiki na dunia mita 1,500 Asbel Kiprop akaambulia nafasi ya 13 (3:58.24). Wakenya Elijah Kiptoo na Andrew Rotich hawakumaliza mashindano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |