Sportpesa Super 8 Premier Ligi Kenya: Kawangware United, Zamalek, TUK zatoka vifua mbele
(GMT+08:00) 2017-05-31 08:36:03
Timu za Kawangware United, TUK na Zamalek zimepata ushindi katika mechi za Sportpesa Super 8 Premier Ligi inayofanyika Nairobi Kenya. Kawangware iliishinda Babete United FC kwa jumla ya magoli 2-1. Nao mabingwa wa zamani timu ya wanafunzi wa chuo kikuu cha ufundi cha Kenya (TUK FC) wamepata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kayole. Kwingineko, Zmalek FC waliibuka na ushindi dhidi ya Ole Rangai FC wa goli 2-1. Matokeo mengine Macmillan FC ilikubali kipigo cha 4-1 toka kwa NYSA FC.