Hadi kufikia usiku wa jana watu 12 wamethibitishwa kufariki kwenye ajali ya moto uliotokea kwenye jengo la makazi mjini London, na idadi ya vifo inatarajiwa kuongezeka. Watu zaidi ya 80 wamepelekwa hospitali.
Waziri mkuu wa Uingereza Bibi Theresa May ameahidi uchunguzi kamili kuhusu ajali hiyo.
Habari nyingine zinasema, wizara ya mambo ya nje ya Morocco imethibitisha kuwa kulikuwa na wamorocco kadhaa kati ya watu waliokumbwa na moto huo, lakini hakuna raia wa Morocco aliyepoteza maisha katika ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |