Takwimu zilizotolewa leo na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR zimeonyesha kuwa,Uganda iliwapokea wakimbizi wengi zaidi duniani mwaka jana, ambapo jumla ya wakimbizi 532,725 waliingia nchini humo, wengi wao wakitokea Sudan Kusini.
Ripoti ya mwaka jana iliyotolewa na shirika hilo inasema, hadi kufikia mwisho wa mwaka huo, watu milioni 65.6 walikimbia makazi yao duniani kutokana na vita na migogoro.
Uturuki ni nchi yenye wakimbizi wengi zaidi duniani, ambao idadi yao imefikia milioni 3.1.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |