Kampuni ya saruji Bamburi Cement ina mpango wa kuongeza uwezo wake wa uzalishaji kutoka tani milioni 2.3 hadi tani milioni 3.3 ili kufikia mahitaji ya soko.
Ongezeko hili litanzia katika kiwanda cha Athi River,ambayo ni ongezeko la tani milioni 0.8 zilizowekwa katika kiwanda cha Mombasa.
Meneja wa miradi ya kiufundi Julius Induswe,akizungumza na waandishi wa habari amesema kampuni imeshawekeza Sh bilioni 4 kuelekea kwa mradi.
Kiasi cha saruji kilichozalishwa nchini kiliongezeka kutoka tani 509,977 kwa mwezi wa Februari 2017 hadi tani 556,883 tani Machi 2017 hii ni kulingana na takwimu za hivi karibuni za serikali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |