Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Geng Shuang amesema, waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang atahudhuria na kuhutubia ufunguzi wa mkutano wa 11 wa baraza la Davos la majira ya joto utakaofanyika kuanzia jumatatu ijayo huko Dalian, China.
Geng pia amesema, waziri mkuu Li atafanya mazungumzo na viongozi wa nchi mbalimbali zikiwemo Finland na Sweden, na wageni wengine kutoka sekta za viwanda, biashara, fedha, akiba ya ujuzi na vyombo vya habari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |