Waziri wa uchumi wa Uturuki Bw. Nihat Zeybekci amesema meli ya kwanza ya Uturuki inayosafirisha misaada kwenda Qatar ilifunga safari jana, kwa lengo la kukabiliana na vikwazo vya mawasiliano dhidi ya Qatar vilivyowekwa na nchi za ghuba. Bw. Zeybekci amesema ndege 105 za mizigo zimesafirisha misaada kutoka Uturuki kwenda Qatar, baada ya nchi kadhaa za ghuba kukata uhusiano wa kidiplomasia na Qatar mapema mwezi huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |